Huduma, Elimu, Utafiti
Muhimbili national . (Namba ya Utambulisho: X0004)
Hospital

Timu ya SADAKA Network kuwatembelea waathirika wa majanga ya moto na ukatili Majumbani baada ya kufanyiwa upasuaji.
Aug 16, 2019


Timu ya SADAKA network ilipata nafasi ya kuwatembelea waathirika wa majanga yatokeayo majumbani pamoja na ukatili baada ya kufanyiwa upasuaji na kuwekewa bandaji Aga khan hospital ikiwa ni miongoni mwa mradi wa “ rudisha tabasamu usoni mwao” ili kuwafariji, na kuwapatia zawadi ya mafuta “ Vaseline skin creams” yaliyotolewa na Unilever Tanzania ili kurahisisha uponaji wao.
Tunatoa shukrani kwa wabia wetu, Aga khan Hospital, RWI foundation, Muhimbili National Hospital, Unilever, Mai consultations and Clouds Media kwa ushirikiano na juhudi walizotoa ilimkufanikisha hili.
Matamanio yetu ni kuona waathirika wote wanapona na kuendelea na kazi zao za kila siku haraka iwezekanavyo.