Ibada ya kwanza
Bwana yesu apewe Sifa,Mimi naitwa Dr.Getrude Rwakatare ,kiongozi mkuu wa makanisa ya mountain of fire Tanzania au mlima wa moto Tanzania leo nataka nikutambulishe kwenye ukurasa wangu wa maombi yenye majibu papo kwa papo.
Pengine unaweza kuwa mbali na kanisa ,pengine unaweza kuwa mkoani ,pengine hata uko nchi nyingine ya mbali ukurasa huu utakusaidia kupata maombi moja kwa moja na majibu yakatokea hapo hapo kwa sababu ni ukurasa mzuri kwa ajili yako.
Kama tunavyojua Mungu hujibu maombi,na kama tunavyojua kuna umuhimu wa kumuomba Mungu yale yote yanayotushinda maana yote yanawezekana kwake yeye aaminiye.