Al Fajir
Kipofu afaidiki kwa mwenye macho kuona, na wala mwenye macho hadhuriki kama kipofu haoni. Kupitia katika Quraan tukufu sura ya 66 aya ya 6, Mwenyezimungu anasema, enyi mlieamini, zikingeni nafsi zenu na nafsi za familia zenu na moto wa Jaanam. Kwani ndani yake kuna Malaika wakali na wenye nguvu ambao hawamuasi Mwenyezimungu kwa yale anayowaamrisha bali wanafanya yale yale ambayo wameamrishwa. Bi maana watakaokua motoni haziwahusu neema za walio peponi, na watakaokuwa peponi hayawahusu mabalaa ya waliokuepo motoni. Hivyo basi tusisahau kumuomba Allah atujaalie mwisho mwema.