KUHUSU SISI

Tupo hapa sio tu kutoa jukwaaa, tupo hapa kuipa sura mpya jamii yetu!

Maendeleo ya jumuiya ni muhimu sana katika kila jamii, panapokuwa na chombo sahihi na msaada hili linaweza kufanyika. Hivyo ndio muhimu sana kuvunja vikwazo vinavyozuia jumuia kuendelea kwa kutambulisha njia ya mawasiliano fanisi na ushirikiano kati ya viongozi ya jumuia, jamii husika na wadau wote.

SADAKA network inatupa chombo pekee kilichotengenezwa kwa  teknolojia ya juu pamoja na muktadha wa ndani pekee kwa idadi ya watu wa nchi husika,kwa kuingiza tamaduni za ndani na mahitaji ya jamii na huku  kuzingatia upatikanaji wa teknolojia ya ndani, kwa dhumuni la kusaidia na kuwezesha jamii.

Jamii husika inajua vizuri changamoto zake na ikiwa na jukwaa la SADAKA network basi sauti zao zitasikiwa kwa urahisi. Kukuwasilisha changamoto zao kupitia jukaa letu, itawasaidia wadau mbalimbali kuweza kuungana kwa pamoja kutatua changamoto hizo kwa ufasaha.

SADAKA network inakuletea kifaa cha kidigitali cha uchangishaji ambacho kita boresha uwazi(kujua  kabla kuhusu taarifa muhimu za mradi kuwa mfuko utafanya nini hasa na kiasi cha pesa kinachohitajika,wadau wanaokuwa kwenye mradi ni kina nani, ufatiliaji na tathmini zipoje na malengo ya mradi ni nini), na kutoa nafasi kwa mfuko unaochangishwa na ufahamu juu ya mradi wa kijamii kuwa katika jukwaa la SADAKA network.

SADAKA network inatoa msaada kwa kila mradi mpaka utekelezaji unapomalizika.

Jukwaa linatoa uwazi na uwajibikaji katika kipengele cha fedha cha miradi, ambayo itajenga uaminifu na tumaini kati ya wafadhili, jamii na wadau wote watakaoshiriki katika kufanikisha lengo.

Tunaimani kubwa kuwa tukichukua mbinu hii ya kuwezesha jamii za ndani kwa kuwasaidia  kuwaleta kwa pamoja viongozi wa jamii husika ,watu maarufu,vyombo vya habari, mashirika yasiyo yakiserikali na wadau mbalimbali kuchukua nafasi chanya katika kujenga ufahamu,kuanzisha na kusimamia miradi yao ya kijamii, tutakua na uwezo wa kuunda athari pana ambayo ni endelevu, ambayo itaboresha kwa kiasi kikubwa maisha ya jamii nyingi za Africa.

               “kila mmoja wetu anaweza fanya tofauti.

                                                             Kwa pamoja tunaweza kufanya mabadiliko.

Dhamira Yetu

Kusaidia jamii ndani ya Africa kwa kuelewa changamoto zao, na kuja na njia ya kuweza kutatua changamoto hizo na miradi endelevu, kwa kuwaleta pamoja wadau ili kutengeneza ufahamu na kutoa msaada unaohitajika juu ya utekelezaji kamili wa suluhisho ikiwa ni katika mipango ya miradi .

  

Dira Yetu

Kuwa na  jamii nyingi endelevu ndani ya Africa, ambapo wataweza kuanzisha, kusimamia na kusaidia miradi ya jamii na kujiendeleza kimarisha kwa kuchukua umiliki na uwajibikaji wao wenyewe wakati ujao.