Hospital Muhimbili national .
Identity Code: X0004
Hospital Aga Khan Health Service, Tanzania
Identity Code: X0001
Shekhe Alhad Salum
Identity Code: A0002
Actress /producer Monalisa .
Identity Code: Y0003
International Foundation Reconstructing Women International (RWI)
Identity Code: X0003
Bishop Jackson Jackson
Identity Code: P0002
Radio Show Maisha Mseto (TIMES FM)
Identity Code: C0011

Put a Smile Back On Their Faces - Press Conference
Nov 08, 2018

Go to Project

Watanzania wameombwa kwa pamoja kushirikiana na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya SADAKA NETWORK , Hospitali ya Muhimbili na Aga Khan kwa kushirikiana na Women to women foundation kuchangia kurudisha tabasamu usoni kwa wakina mama na watoto waliopata matatizo hayo kwa bahati mbaya, kupata ajali,kwa ukatili wa kijinsia, kupigwa au matatizo yoyote yaliyopelekea wao kuharibika maumbile yao ikiwa ni usoni ama sehemu nyengine ya mwili.

Mwanzilishi wa taasisi hiyo Dkt. Ibrahim Msengi akizungumza na waandishi wa habari alisema kuwa gharama za kuwatibu watoto na akina mama ni kubwa na haziwezi kubebwa na Muhimbili au Aga Khan peke yake wala Women to women foundation,bali ghalama hizi zitafanikiwa endapo wananchi wataungana kwa pamoja ili kutoa michango yao ili kufanikisha zoezi hilo.

"Upasuaji huu utafanyika katika Hospitali ya Muhimbili na Aga Khan na tunatarajia kuwafanyia upasuaji watu 40 kutoka sehemu zote Tanzania,hivyo pesa inayohitajika ni Tsh Milioni 268" alisema Dkt. Msengi.